

**LESONI**
Ijumaa ya leo 17 Machi 2017Maandalio ya Sabato ya BwanaTafakari zaidi
Ukweli dhahiri kuwa watu wanauliza kwa shauku endapo wametenda dhambi isiyosameheka hudhihirisha kuwa kwa hakika hawajafanya hivyo. Kama wangelikuwa wameitenda, kwa hakika wasingelihofia jambo hilo. Hofu yao ndio ushahidi hasa wanaouhitaji kwamba, kwa kweli, bado wako tayari kwa ajili ya uongozi wa Roho. Anachotakiwa kufanya mtu huyo ni kudai haki ya Yesu na, kushikilia sifa stahilifu za Yesu, kusonga mbele katika imani na utii. Ni kwa njia ya kufunikwa na haki ya Kristo pekee, ambayo ni “haki ya Mungu” (Rum. 10:3), ndipo anapoweza kupata amani na uhakikisho ambao sasa wanapungukiwa sana.Kwa kweli, kuna mtu mmoja ambaye Mungu hawezi kumsamehe, na huyo ni mtu anayeendelea kukataa kuja kwa Yesu ili aweze kupewa msamaha. “Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu haitokani na neno au tendo lolote la ghafla; lipo katika upinzani thabiti na wa makusudi dhidi ya kweli na ushahidi husika uliotolewa.”— Ellen G. White Comments, The SDA Bible Commentary, vol. 5, uk. 1093. “Hakuna mtu yeyote anayepaswa kuiangalia dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu kama kitu fulani cha siri na kisichoweza kujulikana. Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni dhambi ya kuendelea kukataa kuitikia mwaliko wa toba.”—Ellen G. White Comments, The SDA Bible Commentary, vol. 5, uk. 1093.
Ijumaa ya leo 17 Machi 2017Maandalio ya Sabato ya BwanaTafakari zaidi
Ukweli dhahiri kuwa watu wanauliza kwa shauku endapo wametenda dhambi isiyosameheka hudhihirisha kuwa kwa hakika hawajafanya hivyo. Kama wangelikuwa wameitenda, kwa hakika wasingelihofia jambo hilo. Hofu yao ndio ushahidi hasa wanaouhitaji kwamba, kwa kweli, bado wako tayari kwa ajili ya uongozi wa Roho. Anachotakiwa kufanya mtu huyo ni kudai haki ya Yesu na, kushikilia sifa stahilifu za Yesu, kusonga mbele katika imani na utii. Ni kwa njia ya kufunikwa na haki ya Kristo pekee, ambayo ni “haki ya Mungu” (Rum. 10:3), ndipo anapoweza kupata amani na uhakikisho ambao sasa wanapungukiwa sana.Kwa kweli, kuna mtu mmoja ambaye Mungu hawezi kumsamehe, na huyo ni mtu anayeendelea kukataa kuja kwa Yesu ili aweze kupewa msamaha. “Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu haitokani na neno au tendo lolote la ghafla; lipo katika upinzani thabiti na wa makusudi dhidi ya kweli na ushahidi husika uliotolewa.”— Ellen G. White Comments, The SDA Bible Commentary, vol. 5, uk. 1093. “Hakuna mtu yeyote anayepaswa kuiangalia dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu kama kitu fulani cha siri na kisichoweza kujulikana. Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ni dhambi ya kuendelea kukataa kuitikia mwaliko wa toba.”—Ellen G. White Comments, The SDA Bible Commentary, vol. 5, uk. 1093.
Nakutakia maandalizi mema ya Sabato

