NENO LA LEO

HII NDIYO JUMLA YA MANENO YOTE YAMEKWISHA SIKIWA MCHE MUNGU, NAWE UZISHIKE AMRI ZAKE ! HII NDIYO JUMLA YA MANENO YOTE YAMEKWISHA SIKIWA MCHE MUNGU, NAWE UZISHIKE AMRI ZAKE

Tuesday, 14 March 2017

UBATIZO NA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU

(Yohana 4, Matendo 1, 1 Wakorintho 12)
Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2011, Bruce N. Cameron, J.D. Marejeo yote ya maandiko yametoka kwenye tafsiri ya New International Version (NIV), copr. 1973, 1978, 1984 International Bible Society, isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo. Nukuu kutoka kwenye tafsiri ya Biblia ya NIV inatumika kwa ruhusa ya Wachapishaji wa Biblia wa Zondervan. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Kama huwa una kawaida ya kupokea somo hili kwa njia ya barua pepe na hukulipata kwa juma moja, unaweza kulipata kwa kubofya kwenye

www.lesoni.blogspot.com kwa lugha ya Kiswahili na http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa Roho Mtakatifu unapojifunza.
Utangulizi: Inamaanisha nini “kubatizwa” kwa Roho Mtakatifu? Nilipobatizwa, mchungaji alisema “nakubatiza kwa jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu.” Je, hiyo inakamilisha jukumu? Kinachonishangaza juu ya jambo hili ni kwamba watu wengi wanabatizwa kwa maneno hayo hayo, lakini hawaonekani kujawa sana na Roho katika uzoefu wao wa kidini. Hebu tuzame kwenye somo letu la Biblia ili tujifunze zaidi!
I.                   Kubatizwa Bila Roho Mtakatifu
A.                Soma Luka 1:41-44. Elisabeti ni mama wa Yohana Mbatizaji. Mariamu ni mama wa Yesu. Habari hii inazungumzia nini juu ya Elisabeti na Roho Mtakatifu? (Roho Mtakatifu alimjaa Elisabeti, na akaonekana kumjaa Yohana akingali tumboni kwa sababu Yohana “aliruka kwa shangwe” baada ya kusikika kwa sauti ya mama wa Yesu.)
B.                 Soma Marko 1:4-8. Kwa nini Yohana Mbatizaji hakubatiza kwa Roho Mtakatifu? Mama yake alijawa Roho Mtakatifu, na inaonekana Yohana Mbatizaji pia alijawa Roho Mtakatifu hata kabla hajazaliwa.
1.                  Yohana Mbatizaji alisema kuwa nani atawabatiza watu kwa Roho Mtakatifu? (Yesu.)
2.                  Angalia tena Marko 1:8. Inawezekana kuwa Yohana alibatiza kwa maji na Roho Mtakatifu kwa wakati mmoja?
C.                 Soma Yohana 4:1-2. Je, Yesu aliwabatiza watu kwa Roho Mtakatifu? (Hii inaashiria kuwa Yesu hakumbatiza mtu yeyote moja kwa moja. Lakini, muhimu zaidi ni kwamba, kifungu hakizungumzii jambo lolote kuhusu wanafunzi, chini ya maelekezo ya Yesu, wakibatiza katika jina la Yesu Kristo.)
D.                Soma Matendo 1:4-5. Hii inatufundisha nini kuhusu wanafunzi kubatiza katika jina la Roho Mtakatifu au wao kubatizwa katika jina la Roho Mtakatifu? (Kifungu hiki kinadhihirisha kuwa bado wanafunzi walikuwa hawajabatizwa kwa Roho Mtakatifu. Kwa kuwa Yesu anarejea tukio la siku za usoni, inaonekana wazi kwamba si wanafunzi wala wala watu waliowabatiza walikuwa wamebatizwa kwa Roho Mtakatifu.)
1.                  Je, Yohana Mbatizaji ni nabii wa uongo katika jambo hili? Au, je, Yohana anarejea jambo jingine tofauti anaposema kuwa Yesu “atawabatiza kwa Roho Mtakatifu” (Marko 1:8)?
2.                  Soma Luka 24:49. Yesu anapowaahidi wanafunzi wake katika Matendo 1:4-5 kwamba “atawapelekea” ubatizo wa Roho Mtakatifu, je, hiyo ilitimiza unabii wa Yohana Mbatizaji?

3.                  Sasa jambo la muhimu kwetu leo – jambo hili linazungumzia nini kuhusu endapo ubatizo wa maji pia ni ubatizo wa Roho Mtakatifu? (Hii inatuambia kuwa sio lazima vifanane. Kwa dhahiri havikutendeka katika kipindi cha maisha ya Yesu hapa duniani.)
E.                 Kimsingi hatujui maneno yaliyotumiwa na wanafunzi wa Yesu katika kuwabatiza watu wakati Yesu alipokuwepo hapa duniani. Ikiwa walitumia maneno “katika jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu,” basi hiyo itakuwa wazi kabisa hilo lilikuwa jambo tofauti na kubatizwa katika Roho Mtakatifu. Hebu tusome Yohana 3:3-8. Je, Yesu alifahamu, katika kipindi cha huduma yake, kwamba ubatizo wa Roho Mtakatifu ulikuwa muhimu? (Ndiyo!)
1.                  Ikiwa Yesu alidhani hivyo, je, ilikuwa na mantiki kwa Yesu kuwaelekeza wanafunzi wake kubatiza katika jina la Roho Mtakatifu wakati bado akiwepo hapa duniani?
F.                  Soma Mathayo 28:18-20. Soma vifungu hivi kwa makini. Vinaashiria nini kuhusu endapo wanafunzi wa Yesu walikuwa wakibatiza katika jina la Roho Mtakatifu hapo awali? (Kauli ya Yesu, ambayo ilitolewa baada ya kufufuka kwake, ina ushawishi mkubwa katika jambo hili. Yesu anasema kuwa “nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni.” Matumizi ya maneno, “basi enendeni” yanaashiria kwamba ni kuanzia katika hatua hii pekee ubatizo katika jina la Roho Mtakatifu uliidhinishwa. Hii inaonesha kuwa Yohana Mbatizaji alitabiri kwa usahihi tukio hili, na inaonesha kuwa ubatizo katika jina la Roho Mtakatifu haukuanza hadi baada ya Yesu kuondoka na kurejea mbinguni. Kwa dhahiri hii inatusaidia kuelewa Matendo 1:4-5.)
1.                  Je, kuna mantiki yoyote katika kungojea muda huu? (Soma Warumi 6:3-4. Ubatizo haukutimiza maana yake halisi hadi Yesu alipokufa na kufufuka. Tunapobatizwa majini, tunashiriki katika kifo na ufufuo wa Yesu. Tunakufa pamoja naye kwa ajili ya dhambi zetu. Hii inaandaa mazingira ya sisi kujawa na Roho Mtakatifu. Angalia Warumi 8:3-4. Hii ni sehemu ya “mamlaka” aliyopewa Yesu baada ya kufufuka kwake!)
II.                Filipo na Ubatizo wa Roho Mtakatifu
A.                Soma Matendo 8:5-8. Je, Filipo amejaa uwezo wa Roho Mtakatifu?
B.                 Hebu turuke mafungu kadhaa. Soma Matendo 8:12-13. Nini maoni yako: je, watu wanabatizwa na Filipo kwa Roho Mtakatifu?
C.                 Soma Matendo 8:14-17. Unaelezeaje jambo hili? Kwa dhahiri Filipo amejawa Roho Mtakatifu, lakini bado habatizi katika jina la Roho Mtakatifu?
1.                  Watu hawa “walibatizwaje” kwa Roho Mtakatifu? (Haukuwa ubatizo. Badala yake, Petro na Yohana kwanza “waliwaombea ili wampokee Roho Mtakatifu” na kisha “wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu.”)
D.                Hebu tupitie chanzo cha tatizo. Soma tena Matendo 8:15-16. Hii inaashiria kuwa jambo gani halikwenda vizuri? (Jinsi tatizo lilivyoelezwa inafanya ionekane kwamba ubatizo wa Roho Mtakatifu unatakiwa ufanyike wakati ule ule ubatizo wa maji unapofanyika. Hiyo ndio kanuni.)

1.                  Utagundua kwamba watu waliweza kuona kuwa bado Roho Mtakatifu alikuwa hajawajia wakati wa ubatizo. Waliwezaje kutambua hivyo? Unapoona ubatizo leo, je, unaweza kuelezea juu ya uwepo wa Roho Mtakatifu?
III.             Uthibitisho wa Ubatizo wa Roho Mtakatifu?
A.                Soma Waefeso 5:17-20. Je, unaona ni jambo la ajabu kwamba Paulo analinganisha ulevi na kujawa Roho Mtakatifu? Kwa nini asilinganishe mauaji, tamaa, uzinzi au wizi, na kujawa Roho Mtakatifu?
B.                 Soma Matendo 2:14-17. Kwa nini Petro anaelezea katika tukio la Pentekoste kwamba wanafunzi hawajalewa? Kwa nini ulinganifu ule ule wa ulevi na kujawa Roho Mtakatifu?
1.                  Unajuaje kwamba mtu amelewa? (Ulevi unaathiri uwezo wa mtu kuzungumza na matendo yake yote. Jambo hilo hilo linadhihirika kwa kujawa Roho Mtakatifu!)
C.                 Soma Matendo 19:1-4. Hiki ni kisa kinachofanana. Je, asili ya ubatizo wao iko wazi? (Ndiyo. Ni ubatizo wa toba wa Yohana Mbatizaji. Hata hawafahamu habari za Roho Mtakatifu.)
D.                Soma Matendo 19:5-7. Je, wanaume hawa walibatizwa upya, au Paulo aliweka tu mikono yake juu yao?
1.                  Tuna uthibitisho gani kwamba walijawa Roho Mtakatifu? (“Walinena kwa lugha na kutabiri.”)
E.                 Soma Matendo 7:55, Luka 1:67, Matendo 2:4, Matendo 4:31 na Matendo 13:52. Tunaona uthibitisho gani wa kujazwa Roho Mtakatifu katika hivi vifungu? (Tunaona maono, unabii, kunena kwa lugha, kupeleka injili kwa ujasiri, na kujaa furaha.)
F.                  Soma 1 Wakorintho 12:4-7. Jambo gani linatolewa “kwa manufaa ya wote?” (Ufunuo wa Roho Mtakatifu.)
              


Je, “kumdhihirisha” Roho Mtakatifu ni sawa na “kujawa” Roho Mtakatifu? (Nadhani. Kama sio sawa kabisa, basi vinaonekana kukaribiana sana. Kama “umejawa” unapaswa “kudhihirisha.”)
G.                Soma 1 Wakorintho 12:8-11. Tunawezaje kufahamu kwamba tumebatizwa kwa usahihi kwa Roho Mtakatifu? Tunawezaje kufahamu kwamba tumejawa Roho Mtakatifu? (Tutadhihirisha mojawapo au nyingi ya hizi karama za roho.)
1.                  Sitakuhitaji usome vifungu sasa hivi, lakini kuna hoja zinazojengwa juu ya vifungu vya Agano Jipya kwamba uthibitisho wa kujawa Roho Mtakatifu ni kuwa na uwezo wa kunena kwa lugha. Kunena kwa lugha ni miongoni mwa karama zilizoorodheshwa ambazo tumezisoma. Je, 1 Wakorintho 12:11 inatufundisha nini juu ya hii hoja? (Inasema kuwa karama za roho, kama vile kunena kwa lugha, zinatolewa na Roho Mtakatifu, “kama apendavyo yeye.” Hiyo inamaanisha kuwa si wote tutakaokuwa na karama inayofanana.)
2.                  Sasa swali gumu: je, umedhihirisha mojawapo kati ya hizi karama za roho? Angalia orodha kwa makini kabla hujajibu.

H.                Rafiki, ikiwa huna uhakika kama umejawa na Roho Mtakatifu, kwa nini usimwombe mtu aliyejawa Roho Mtakatifu akuwekee mikono ili kutatua tatizo hilo? Kama bado hujabatizwa, kwa nini usiombe kubatizwa katika jina la “Baba, Mwana na Roho Mtakatifu?”

IV.    Juma lijalo: Roho Mtakatifu na Kuishi Maisha Matakatifu.

No comments:

Post a Comment